Sunday, February 18, 2018

Polisi 6 wakamatwa kufuatia kifo cha mwanafunzi Akwilina Akwiline Tanzania


Maafisa sita wa polisi wamekamatwa kuhusiana na kifo cha mwanafunzi wa chuo cha kitaifa cha usafirishaji Akwilina Akweline.
Hayo ni kwa mujibu wa kamanda wa sehemu maalamu mjini Dar es Salaam Lazaro Mambosasa wakati wa mkutano na wanahabari uliofanyika siku ya Juamapili.
Mambosasa pia alibaini kwamba maafisa wa polisi wanachunguza maafisa wengine 40 kuhusiana na kifo hicho.
Mwanafunzi huyo ambaye alikuwa mwaka wa kwanza katika chuo hicho ambaye jina lake lilisambazwa katika mitandao ya kijamii aliripotiwa kupigwa risasi alipokuwa ndani ya basi siku ya Ijumaa.
Shirika la wanafunzi nchini limemtaka waziri wa maswala ndani nchini humo Mwigulu Nchemba kuchukua jukumu la kisiasa na kujiuzulu kufuatia kisa hicho.
Akizungumza na wanahabari, mwenyekiti wa shirika hilo Abdul Nondo alisema kuwa iwapo Mwigulu hatojiuzulu basi watamtaka rais John Pombe Magufuli kumfuta kazi.
''Kufuatia mauaji na kutoweka kwa watu kadhaa ni wakati kwamba bwana Mwigulu anafaa kuchukua jukumu na kujiuzulu'', alisema.
Wakati huohuo Serikali imesema kuwa itagharamika kusimamia mazishi ya mwanafunzi huyo.
Akizungumza mjini Dar es Salaam waziri wa elimu, Sayansi na Teknolojia Joyce Ndalichako alisema kuwa Akwilina aliuawa wakati alipokuwa akielekea Bagamoyo.
''Aliuawa alipokuwa akielekea Bagamyo kuwasilisha ombi lake la kutaka kupewa mafunzo kwa vitendo'', alisema.
Kwa upande wake naibu waziri wa maswala ya Tanzania Hamad Masauni amesema kuwa serikali itahakikisha kuwa uchunguzi kuhusu kisa hicho unafanyika mara moja ili washukiwa washtakiwe.

Wednesday, February 14, 2018

Morgan Tsvangirai afariki dunia



Kiongozi mkuu wa upinzani nchini Zimbabwe Morgan Tsvangirai amefariki dunia nchini Afrika kusini.

Kwa mujibu wa kiongozi Mwandamizi wa chama cha MDC, Tsvangirai mwenye umri wa 65, na aliyewahi kushika nafasi ya Uwaziri mkuu nchini Zimbabwe ameripotiwa kuwa alikuwa akisumbuliwa na Saratani ya utumbo.

Makamu Rais wa chama chama cha MDC Elias Mudzuri ameliambia Shirika la Habari la Uingereza Reuters kwamba marehemu alifariki jioni ya Februar 14.

Katika kipindi cha uhai wake, maisha yake ya kazi yaligubikwa na harakati nyingi za kisiasa dhidi ya mpinzani wake Rais wa zamani wa Zimbabwe Robert Mugabe



Aliwahi kupigwa na kufungwa mara kadhaa.
Morgan Tsvangirai alianzisha chama cha Movement for Democratic Change -MDC- mwaka 2000, na kuanza kutoa changamoto kwa Rais wa zamani wa nchi hiyo aliyekaa madarakani muda mrefu.
Kufuatia kifo hicho Bwana Tsvangirai . MDC inaelekea kugawanyika juu ya nani atakayeongoza uchaguzi hapo baadaye mwaka huu dhini ya chama tawala cha Zanu PF, ambacho kwa sasa kinaongozwa na Emmerson Mnangagwa.

bbc...

Zuma ajiuzulu






Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma ameamua kujiuzulu mara moja kufuatia kuongezeka kwa shinikizo kutoka kwa chama chake, kinachotawala nchini humo cha African National Congress, ANC.
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma hatimaye ameamua kujiuzulu jana Jumatano, baada ya kushinikizwa na chama chake, kinachotawala nchini humo cha African National Congress, ANC, kufuatia miaka 9 ya kukabiliwa na kashfa za rushwa, kuporomoka kwa uchumi na kushuka kwa umaarufu.
Zuma alikilalamikia chama cha ANC kwa kumtaka aondoke madarakani, ikiwa ni pamoja na kumtishia kumuondoa kupitia kura ya bunge ya kutokuwa na imani naye, iliyopangwa kupigwa hii leo, Alhamisi.
Rais Zuma amesema ataheshimu maagizo ya chama chake cha ANC kwa kujiuzulu wadhifa wake, baada ya wiki kadhaa za uvumi kuhusu mustakabali wake. Alinukuliwa akisema “nimeamua kujiuzulu kutokana na kura ya kutokuwa na Imani iliyokuwa imepangwa kupigwa siku ya Alhamisi".
Katika hotuba ya kitaifa aliyoitoa kwa dakika 30 kupitia tekevisheni, Zuma alisema, hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja. 
Zuma amekuwa katika mvutano wa kimadaraka na mfanyabiashara bilionea wa zamani na makamu wa rais, Cyril Ramaphosa ambaye sasa anakuwa rais wa mpito. Ramaphosa aliyeshinda nafasi ya kukiongoza chama cha ANC, baada ya kuchaguliwa mwezi Disemba, atapigiwa kura na wabunge nchini humo kuwa rais mpya ama leo au kesho Ijumaa. 
dw..

Tuesday, February 13, 2018

ANC yamshinikiza Jacob Zuma ajiuzulu







Chama tawala nchini Afrika Kusini bado kinaendelea kumshinikiza Rais Jacob Zuma aachie madaraka kwa hiyari yake, baada ya kiongozi huyo anayekabiliwa na kashia kadhaa za kifisadi kukataa kujiuzulu.
Viongozi wa chama tawala nchini Afrika Kusini cha African National Congress, ANC, katika kikao chao kilichomalizika usiku wa kuamkia leo wamefikia makubaliano kuwa Rais Zuma lazima ang'oke madarakani.
Halmashauri Kuu ya ANC yenye wajumbe 107 ilikutana kwa masaa 13 katika hoteli moja nje ya mji wa Pretoria na kupitisha uamuzi huo wa kumtaka Zuma aondoke madarakani.
Vyombo vya habari vingine vimeripoti kuwa chama cha ANC kitamuandikia Zuma kikimuamuru kujiuzulu kama rais wa nchi hiyo baada ya ombi lake la kutaka kuendelea kusalia madarakani kwa miezi kadhaa kukataliwa.
Shirika la Utangazaji la nchi hiyo, SABC, limesema chama cha ANC kimempatia Zuma masaa 48 kuwa tayari amewasilisha barua yake ya kujiuzulu. Hata hivyo, maafisa wa chama hicho hawakupatikana kuthibitisha taarifa hizo, ingawa chama hicho kimeitisha mkutano na waandishi wa habari baadaye hii leo katika makao makuu ya chama hicho mjini Johannesburg.
Chama cha ANC kinaweza kumlazimisha Zuma ajiuzulu lakini mamlaka hayo yanaishia katika ngazi ya chama tu na habanwi na katiba ya nchi hiyo  kulazimika kujiuzulu.
Iwapo atakataaa kujiuzulu, basi huenda akaondolewa madarakani kupitia bunge kwa kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye. Hoja ya upinzani dhidi ya Zuma ya kumpigia kura ya kutokuwa na imani naye inayoungwa mkono imepangwa kufanyika Februari 22 lakini wafadhili wa hoja hiyo wanataka hoja hiyo irejeshwe wiki hii.
Wakati shinikizo la kumuondoa Zuma madarakani likizidi kupamba moto, mwenyekiti wa ANC, Cyril Ramaphosa,  inaripotiwa aliondoka katika kikao cha jana usiku na kwenda kuzungumza ana kwa ana na Rais Zuma katika makao yake rasmi mjini Pretoria lakini hata hivyo msafara wa magari wa Ramaphosa ulionekana ukirejea katika mkutano huo jana usiku na saa tatu baadaye mkutano huo ulimazika.
Cyril Ramaphosa anayetarajiwa kushika madaraka ya urais pindi Zuma atakapoaoondoka madarakani amekuwa  akifanya mazungumzo na rais Jacob Zuma  tangu alipokataa ombi la viongozi wa chama hicho la kumtaka kujiuzulu zaidi ya wiki moja iliypita.
Mkwamo huuu wa kisiasa nchini Afrika Kusini umeiingiza nchi hiyo katika mashaka makubwa kiutawala  na kushindwa kujua nani hasa kwa sasa anaongoza nchi hiyo mnamo wakati pia matukio muhimu ya kitaifa yakifutwa ikiwemo hotuba ya kila mwaka ya kitaifa katiba bunge la nchi hiyo iliyokuwa itolewe Alhamisi iliyopita.
Akihutubia mkutano wa hadhara wa chama cha ANC  jumapili mjini Capetown, Cyril Ramaphosa mwenye umri wa miaka 65, huku akishangiliwa aliwaeleza wanachama wa ANC kuwa yeye na viongozi wenzake wanatambua juu ya shauku walio nayo ya kutaka suala hilo limalizike haraka na kuwaahidi  kuwa halimashauri kuu ya chama  haitawaangusha na itafanya kwa ufasaha jambo hilo.
Zuma ambaye alichukua madaraka mwaka 2009 na  akiwa katika muhula wake wa pili na wa mwisho ameomba apewe ulinzi kwa familia yake pamoja , kulipiwa gharama za kisheria  na kuruhusiwa kukaa madarakani miezi kadhaa kama sharti la kumtaka aondoke madarakani. Hiyo ni kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini Afrika Kusini.
DW.

Friday, February 2, 2018

Mzee Kingunge Ngombale Mwiru afariki dunia Tanzania



Mzee Kingunge amekuwa akitibiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Mwanasiasa huyo mkongwe alilazwa hospitalini mwanzoni mwa Januari akiuguza majeraha ya kushambuliwa na kung'atwa na mbwa nyumbani kwake 22 Desemba mwaka jana na akafanyiwa upasuaji.
Rais John Magufuli amesema apokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha Mzee Kingunge na kusema alikuwa mtu aliyechangia katika juhudi za kupigania uhuru wa Tanzania na na baada ya uhuru awaka mtumishi mtiifu wa chama cha Tanu na baadaye CCM.
"Ametoa mchango mkubwa sana, sisi kama taifa hatuwezi kusahau na tutayaenzi mema yote aliyoyafanya wakati wa utumishi wake uliotukuka," amesema Dkt Magufuli kupitia taarifa.
"Ametuachia somo la kupigania maslahi ya nchi wakati wote, kuwa wazalendo wa kweli, kudumisha Amani na mshikamano, kuchapa kazi kwa juhudi na maarifa na kuwa na nidhamu."
Viongozi pia wametuma salamu zao za rambirambi na kumuomboleza mwanasiasa huyo akiwemo kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe.
Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki kutokaTanzania wanaomboleza kuondokewa na mwanasiasa huyo na kusema atakumbukwa kwa mchango wake katika maendeleo ya Afrika Mashariki.
"Ametoa mchango mkubwa na ni muumini wa uanajumuiya wa Afrika na siasa za ukanda. Ndugu Kingunge siku zote alisimamia muungano na umoja na alipinga sana utengano. Mzee Kingunge aliamini katika mshikamano na ushirikiano," wamesema kupitia taarifa.
Mzee Kingunge alikuwa mmoja wa viongozi wa muda mrefu na miongoni wa watu waliokuwa na ushawishi katika Chama cha Mapinduzi (CCM) hadi alipojiuzulu kutoka kwenye chama hicho Oktoba 2015 akilalamikia alichosema ni ukiukaji wa katiba ya chama hicho.
Kabla ya kujiuzulu, alikuwa amesema kwamba hakuwa amefurahishwa na utaratibu uliotumiwa kumteua mgombea urais wa CCM mjini Dodome Julai mwaka huo.
Hata hivyo, aliahidi kutohamia chama kingine.
Bw Kingunge alikuwa amehduumu katika CCM tangu kuanzishwa kwa chama hicho mwaka 1977.
Mke wake, Peras, alifariki dunia mwezi uliopita akitibiwa pia Muhimbili baada ya kulazwa kwa miezi kadha.
Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli alikuwa amefika katika Wodi ya Mwaisela iliyopo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kumjulia hali Mzee Kingunge mwanzoni mwa mwezi Januari.

Wednesday, January 31, 2018

Arsenal yakamilisha uhamisho wa Aubameyang



Pierre-Emerick Aubameyang sasa ni mchezaji wa Arsenal, klabu hiyo ya London  imetangaza hili.
Aubameyang ametia saini mkataba wa "muda mrefu kwa uhamisho ambao umevunja rekodi ya klabu" kutoka Borrussia Dortmund.
"Mchezaji wetu wa pili wetu kumnunua wakati wa kipindi cha kuhama wachezaji Januari. Auba ni miongoni mwa washambuliaji stadi zaidi duniani. Amefunga mabao 98 katika mechi 144 akichezea klabu ya Dortmund ligi ya Bundesliga na amesaidia ufungaji wa mabao 172 katika mechi 213 ambazo ameshiriki akichezea klabu hiyo yake ya zamani michuano yote," Arsena wameandika kwenye mtandao wao.
Dortmund ilikuwa imesema kuwa itamuuza mcheza huyo baada ya kupata mbadala wake huku mshambuliaji wa Chelsea Michy Batshuayi akitarajiwa kujiunga na klabu hiyo kwa mkopo.
Aubameyang alifunga mabao 141 katika mechi 213 akiichezea Dortmund tangu 2013, ikiwemo mechi 21 kati ya 24 msimu huu.
Lakini alipigwa marufuku na klabu hiyo ya Ujerumani katika mechi yao dhidi ya Wolfsburg tarehe 14 Januari kwa kukosa mkutano wa timu.
Mshambuliaji huyo pia aliwachwa nje kwa mechi yao dhidi ya Hertha Berlin kwa sababu maafisa wa klabu hiyo walihisi hakuwa na malengo lakini alicheza dakika 90 katika mechi ya Jumapili dhidi ya Freiburg.
Ameichezea Gabon mara 56 akifunga magoli 23.

Tuesday, January 30, 2018

MECHI ZA LEO TAREHE 31/01/2018 EPL

Chelsea 19:45 AFC Bournemouth

 Everton 19:45 Leicester City

Newcastle United 19:45 Burnley

Southampton 19:45 Brighton & Hove Albion

Manchester City 20:00 West Bromwich Albion

Stoke City 20:00 Watford

Tottenham Hotspur 20:00 Manchester United

Arsenal walazwa na Swansea City EPL



Swansea City waliondoka kwenye eneo la hatari ya kushushwa daraja Ligi ya Premia kwa mara ya kwanza tangu Novemba baada ya kuwalaza Arsenal.
Kosa la ajabu kutoka kwa Petr Cech lilimpa nafasi Jordan Ayew kufunga bao na kuwaweka wenyeji kifua mbele kipindi cha pili kabla ya Sam Clucas kufunga bao lake la pili usiku wa Jumanne na kukamilisha ushindi wao wa 3-1.
Mesut Ozil alikuwa ametoa pasi safi na kumuwezesha Nacho Monreal kufunga bao la kwanza mechi hiyo dakika ya 33 kabla ya Clucas kuwasawazishia Swansea uwanjani Liberty Stadium dakika moja baadaye.
Swansea wameandikisha ushindi mtawalia mara ya kwanza msimu huu.
Vijana wa Arsene Wenger nao wameshinda mechi moja pekee kati ya 13 walizocheza ugenini msimu huu Ligi Kuu ya England.
"Najihisi kwamba kwa kujilinda leo tulikuwa dhaifu sana na tulifanya makosa makubwa. Vyema zaidi ni kutozungumzia bao la pili na la tatu," alisema Wenger baada ya mechi.
"Swansea walikuwa makini sana, wenye nidhamu na hamu ya kutaka kushinda. Nasikitika, na naamini kwamba hatukucheza kwa kiwango cha kutosha, naamini hatukuwa na nidhamu ya kutosha.
Swansea wameonekana kuimarika sana chini ya meneja mpya Carlos Carvalhal ambapo wameshindwa mechi moja pekee kati ya nane walizocheza.
Ushindi wao dhidi ya Arsenal ndio wao wa pili mtawalia dhidi ya klabu iliyo nafasi sita za juu kwenye jedwali.
Liverpool ambao wamekuwa wakifunga mabao sana msimu huu walizimwa Liberty Stadium pia..
Huku Gunners wakitatizika Liberty Stadium, kulikuwa na wasiwasi na utata zaidi kuhusu shughuli za Wenger soko la kuhama wachezaji mwezi huu.
Arsenal wanatumai watafanikiwa kumnunua Pierre-Emerick Aubameyang kabla ya soko kufungwa leo jioni, lakini hiyo itategemea Mfaransa Olivier Giroud kuhama kutoka Emirates kwenda Stamford Bridge.
Giroud alijumuishwa kikosi cha Arsenal, lakini alikaa benchi pamoja na Henrikh Mkhitaryan.
Mashabiki waliimba jina lake kipindi chote cha mechi na bila shaka atakoswa sana na baadhi ya mashabiki wa Gunner iwapo ataondoka.

Manchester City sign French defender for club record £57m


Manchester City have signed French defender Aymeric Laporte from Athletic Bilbao for a club record fee of £57m.
The fee for Laporte, yet to win a cap for France, takes spending by Premier League clubs to £252m this month - a record for a January transfer window.
And the 23-year-old's arrival takes City's spending on defenders since the end of last season to £190m.
The club's previous record fee was the £55m paid to Wolfsburg for Belgium midfielder Kevin de Bruyne in 2015.
The centre-back has played 19 times for France at Under-21 level.
"I am looking forward to working under manager Pep Guardiola and trying to help the club to achieve success," he told the City website.
"It means a lot that the club have shown faith in me and I am excited to get started."
Injury concern over skipper Vincent Kompany and uncertainty over the reliability of Eliaquim Mangala led Guardiola to believe he required another central defender in addition to current first choices John Stones and Nicolas Otamendi.
bbc.

Raila 'aapishwa' kuwa 'rais wa wananchi' Kenya




Kiongozi mkuu wa upinzani nchini kenya bwana Raila Odinga amejiapisha kuwa raisi wa wananchi kenya, huku serikali ikifungia baadhi ya vituo vya habari vilivyokuwa vinapeperusha matangazo ya moja kwa moja.
bbc.



DANIEL STURRIDGE AJIUNGA KWA MKOPO WBA

Mshambuliaji wa Liverpool Daniel Sturridge amejiunga kunako timu ya  West Bromwich Albion kwa mkopo.

Football transfer news and rumours live: Will the Pierre-Emerick Aubameyang saga reach a conclusion?





It seems the world and his dog are chasing a new striker this January, and we start with the extraordinary transfer merry-go-round that threatens to define the whole window.
As revealed in a Telegraph Sport exclusive on Monday morning, Arsenal have agreed a club record £55.4 million deal with Borussia Dortmund for their top goalscorer Pierre-Emerick Aubameyang.
Arsenal fans reaching for the champagne might want to think twice however, as the German club need to acquire a replacement before signing off on the transfer.

Polisi 6 wakamatwa kufuatia kifo cha mwanafunzi Akwilina Akwiline Tanzania

Maafisa sita wa polisi wamekamatwa kuhusiana na kifo cha mwanafunzi wa chuo cha kitaifa cha usafirishaji Akwilina Akweline. Hayo ni k...